Katibu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ndg. Baraka Leonard, amekutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Jukwaa la Mabunge ya Nchi Wanachama wa Ukanda wa Maziwa Makuu (FP-ICGLR), Mhe. Balozi Dkt. Deo Mwapinga alieambatana na ujumbe wake walipomtembelea tarehe 29 Januari, 2026 Ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma.