Habari
Mkutano wa Tatu wa Bunge waanza Bungeni Jijini Dodoma
Mkutano wa Tatu (3) wa Bunge la 13, umeanza Jumanne tarehe 31 Machi, 2026 Jijini Dodoma. Mkutano huu ni mahsusi kwa ajili ya kujadili utekelezaji wa Bajeti za Wizara zote kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026 pamoja na Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027.
Shughuli nyingine zitakazofanyika katika Mkutano huo ni kama ifuatavyo:-
Aidha, katika Mkutano huu wa Bunge, jumla ya Miswada minne itawasilishwa Bungeni ambayo ni:-
Muswada wa Sheria ya Fedha za Matumizi ya Serikali wa Mwaka 2026 (The Appropriation Bill, 2026) utapitishwa kwa hatua zote;
Muswada wa Sheria ya Fedha wa Mwaka 2026 (The Finance Bill, 2026);
Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali wa Mwaka 2026 [The Written Laws (Miscellaneous Amendments) Bill, 2026]; na
Muswada wa Sheria ya Mikopo kwa Dhamana za Mali zinazohamishika wa Mwaka 2026.
Pia katika Mkutano huu jumla ya maswali ya kawaida 845 yanatarajiwa kuulizwa na kujibiwa Bungeni. Aidha, wastani wa maswali 104 ya papo kwa papo kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu yataulizwa na kujibiwa siku za Alhamisi.
Vile vile wakati wa Mkutano huu, kutakuwa na Uchaguzi wa Wabunge wawili wa Bunge la Afrika Mashariki kuziba nafasi zilizowazi baada ya Mheshimiwa James Kinyasi Millya na Mheshimiwa Dkt. Ngwaru Jumanne Maghembe kuchaguliwa kuwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025. Tangazo la Uchaguzi huo litatangazwa kwenye Gazeti la Serikali na tarehe ya Uchaguzi huo itatolewa rasmi baada ya taratibu zote kukamilika.
