United Republic of Tanzania
Parliament of Tanzania

Spika wa Bunge la Tanzania Mhe. Job Ndugai amesema ili Bara la afrika
liweze kuwa Bara lenye nguvu kiuchumi na sauti ya maamuzi duniani halina
budi kujikita katika umoja na mshikamono.
Mhe. Ndugai aliyasema hayo alipokuwa akilihutubia Bunge la Afrika (Pan
African Parliament) leo kuwasilisha Ujumbe wa Mshikamano kwa wabunge wa
Bunge hilo wakati wa Ufunguzi wa rasmi wa Mkutano wa Pili wa Bunge hilo
uliofanyika Mjini Midrand Afrika Kusini.
Akizungumzia changamoto zinazolikabli bara la Afrika Mhe. Nduagi alisema
nchi nyingi barani Afrika zinakabiliwa na matatizo yanayolingana ambayo
ni Vita vya wenyewe kwa wenyewe, ugaidi, umasikini na mengineyo ambayo
yanahitaji suluhisho la Pamoja kuyakabili..
“ katika duniani ya sasa ni vyema tukakabiliana na changamoto
zinazotukabili kwa pamoja. Matajiri hawawezi kuepuka athari za umasikini
na ukosefu wa amani. Kinachotokea eneo moja kinaathiri maeneno mengi
mathalani vita vya wenyewe kwa wenyewe Somalia imesababisha wakimbizi
katika maeneo mengi duniani” alisema Ndugai
Akizungumzia nafasi ya wabunge katika kupiga vita changamoto
zinazolikabili bara la Afrika, Mhe. Ndugai amesema wabunge wa Bunge la
Afrika kama wawakilishi wa Manbunge ya Nchi wanachama wa Umoja wa Afrika
wanawajibu wa kutetea maslahi ya Bara la Afrika bila kujali itikadi za
kisiasa, maeneo wanayotoka na mambo mengine yanayoweza kuligawa bara la
Afrika.
“ Mkiwa Wabunge mnaowakilisha nchi zenu katika Bunge hili, nilazima
mhakikishe Umoja wa Afrika unasimamia ipasavyo masalahi ya bara la
Afrika ili kutimiza ndoto waliokuwa nayo waasisi wa umoja huu wa Afrika.
Kwa mfano baba wa Taifa la Tanzania Mwalimu Julius kambarage Nyerere
alisema lazima tukimbie wakati wengine wakitembea” aliongeza Ndugai
Mapema akitoa salamu za Bunge la Lesotho, Spika wa Bunge la Nchi hiyo
Mhe. Nthloi Motsamai alisifu juhudi za Mwalimu Julius Nyerere pamoja na
waasisi wengine wa bara hili katika kuimarisha umoja wa Afrika na
kuwataka wabunge wa Bunge la afrika kuhakikisha mawazo ya viongozi hawa
ya kulifanya bara la afrika kuwa moja yanatimia.
Katika hatua nyingine, wabunge wa Tanzania wanaowakilisha Tanzania
katika Bunge la Afrika walikula kiapo cha uaminifu kuwa wabunge wa Bunge
hilo baada ya Bunge la Tanzania kuwachagua mapema mwezi Januari.
Wabunge hao ni pamoja na Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile, Mhe. Mboni Mhita,
Mhe. David Silinde na Mhe. Asha Abdalah Juma. Mhe. Ndugai anatarajia
kurejea nchini kesho jumatano ambapo Bunge la Afrika linaendelea na
Vikao vyake hadi tarehe 13 Mei, 2016.