|
|
| Home »Supplementary Question |
| |
 |
E-mail this to a friend |
 |
Printable version |
 |
Ole-Sendeka, Christopher Olonyokie[CCM]
Simanjiro Constituency |
|
|
|
|
|
|
| 16 |
10 |
GOOD GOVERNANCE |
Corruption |
10 June 2009 |
Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Waziri nina maswali madogo ya nyongeza:-
Kwa kuwa utashi wa kisiasa wa kupambana na vita dhidi ya rushwa unaweza pia kupimwa na hatua zinazochukuliwa dhidi ya wale ambao wamekuwa wakituhumiwa katika mchezo huu mchafu wa rushwa.
(a) Je, Serikali inasemaje kuhusu kuchukua hatua za haraka kuwafikisha Mahakamani wale wote ambao wamehusika kwa namna moja ama nyingine kwenye mikataba ambayo ina harufu ya rushwa ikiwemo ya Richmond, IPTL, EPA na mengine ambayo haiiweki nchi yetu katika sura nzuri katika uso wa dunia?
(b) Kwa kuwa kumekuwepo na dalili kwamba mikataba kama ya Madini na mikataba mbalimbali ambayo Serikali yetu imekuwa ikiingia baadaye ndiyo tunakuja kugundua kwamba kuna harufu ya rushwa katika mikataba hiyo:-
Je, ndiyo tuseme kwamba katika Taasisi muhimu kama BOT na katika kuingia mikataba hiyo Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa au PCCB haipo katika Benki Kuu kiasi kwamba inaweza kutokea ufisadi kama ule uliotokea? Pengine labda niweke vizuri swali hili Mheshimiwa Spika.
Pengine tunachukua hatua gani za kukinga badala ya kuhangaika kutibu ili tuiweke nchi yetu katika sura nzuri katika uso wa dunia?
|
| ANSWERS TO SUPPLEMENTARY QUESTION # 10
SESSION # 16 |
 |
Answer From Hon.Simba, Sophia Mattayo
GOOD GOVERNANCE |
|
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (UTAWALA BORA):
Mheshimiwa Spika, namshukuru Mheshimiwa Ole-sendeka, kwa maswali yake na naomba nimjibu kama ifuatavyo:-
Kuhusu hatua zinazochukuliwa kuwafikisha Mahakamani wale wote waliohusika na kesi mbalimbali nadhani yeye anatambua kwamba Serikali inafutia kesi zote hizi kwa karibu sana lakini ufuatiliaji wa kesi mbalimbali za rushwa unaongozwa na Sheria ya rushwa ambayo inakataza kabisa kuzungumzia mwenendo wa uchunguzi wa kesi yoyote.
Kuzungumzia mwenendo wowote wa kesi kabla haijafika Mahakamani na hata ikifika Mahakamani ni kosa la jinai. Kwa hiyo, kwa hapa sitoweza kumpa majibu kwamba tumefikia wapi na kesi ya IPTL na EPA. EPA iko Mahakamani na yeye anatambua hiyo. Siwezi kuzungumzia Richmond hiyo iko katika hatua mbalimbali na kwa kiasi kikubwa anaelewa kwamba masuala ya Richmond yamekuwa kidogo yana utata kutokana na kwamba Richmond wenyewe katika mchakato mzima hawakupata hata senti Tano. Haijalipwa, kwa hiyo hakuna hata pesa ambayo imepita na kwenye rushwa lazima kuonyesha Consideration ambayo imetolewa katika parties ambazo zinahusikana na rushwa. Kwa hiyo, bado tuna kitendawili ambacho tunaendelea kukishughulikia na siwezi katika hatua hii kuzungumzia masuala haya.
Mheshimiwa Spika. Swali lake la pili anazungumzia mikakati kuhusu mikataba mbalimbali ambayo inaingiwa na Benki Kuu na vyombo vyetu vingine. Ni kweli sote tunafahamu kwamba, wenzetu ambao walipewa dhamana ya kuingia mikataba mbalimbali walikuwa hawana utaalamu wa kutosha na hivyo kutuingiza katika matatizo makubwa. Lakini Serikali inachukua kila hatua ya kuhakikisha kwamba matatizo haya ya kuingia kwenye mikataba ambayo haina manufaa na nchi yetu yanapewa Wataalamu ambao kwa sasa Serikali inafanya jitihada ya kutoa mafunzo ya kiutaalamu jinsi ya kuingia katika mikataba hii. Nashukuru.
|
|
Records 1 to 1 of 17 |
|
|
|
|
|