|
|
| Home »Principal questions |
|
| |
 |
E-mail this to a friend |
 |
Printable version |
 |
Honourable Job Yustino Ndugai [CCM]
Kongwa Constituency |
|
| 9 |
112 |
LIVESTOCK DEVELOPMENT |
Livestock |
8 November 2007 |
Kwa kuwa, ni nia ya Serikali kuendeleza na kuimarisha ujenzi wa miundombinu ya mifugo kama majosho, malambo na kadhalika.
Je, kwa mwaka 2006/2007, ni majosho mangapi na malambo mangapi yaliyo maeneo gani yamejengwa katika Wilaya za Kongwa na Mpwapwa?
|
| ANSWERS TO PRINCIPAL QUESTION #112 SESSION # 9 |
 |
Answer From Hon. Mlingwa, Dr. Charles Ogesa F.
LIVESTOCK DEVELOPMENT |
|
NAIBU WAZIRI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Job J. Ndugai, Mbunge wa Kongwa, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, nakubaliana na Mheshimiwa Mbunge kwamba ni nia ya Serikali kuona kwamba miundombinu ya mifugo imefanya kazi ipasavyo.
Serikali inafanya hivyo kwa kiasi kikubwa kupitia Mamlaka ya Serikali za Mitaa na kwa kushirikiana na wananchi na sekta binafsi. Kuanzia mwaka 2003/2004, Serikali ilibuni mipango ya maendeleo ya kilimo Wilayani (DADPs), ambapo Wilaya huibua miradi mbalimbali kwa njia shirikishi ikiwa ni pamoja na ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya mifugo kama vile majosho na malambo.
Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2006/2007, Wilaya ya Mpwapwa ilikarabati josho la Mbuga kwa jumla ya shilingi milioni 5 na lambo la Iyenge kwa jumla ya shilingi milioni 10. Wilaya ya Kongwa kwa upande wake haikuwasilisha maombi ya ujenzi au ukarabati wa majosho na malambo kwa mwaka 2006/2007 kwa kuwa ilikuwa na vipaumbele vingine.
Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2007/2008, Wilaya za Kongwa na Mpwapwa zimewasilisha maombi ya kukarabati miundombinu ya mifugo kama ifuatavyo:-
Wilaya ya Kongwa itajenga josho jipya moja la Chitego kwa gharama ya Sh.12,000,000= na kukarabati majosho sita ya Hogolo Sh.3,500,000/=. Nagesemi (Sh.2,500,000/=), Kongwa (Sh.2,500,000/=), Laikali (Sh.2,500,000/=), Pandambili (Sh.4,500,000/=) na Mseta - Bondeni (Sh.2,500,000/=). Wilaya ya Mpwapwa itajenga majosho manne ya Msagali, Kimagai, Kikuyu na Lufu kwa gharama ya Sh.49,500,000/= na pia itakarabati majosho matatu ya Mwanawota, Winza na Kisima kwa gharama ya Sh.19,500,000/=.Aidha, Wilaya ya Mpwapwa pia imetenga Sh.85,500,000/= kwa ajili ya malambo ya Sazima, Mzase, Kibakwe na Lukole.
Mheshimiwa Spika, napenda kuwapongeza wananchi wa Wilaya za Kongwa na Mpwapwa kupitia Waheshimiwa Wabunge wao kwa kuibua miradi ya kujenga na kukarabati miundombinu hii ya mifugo kwa lengo la kuboresha sekta ya mifugo na naomba waendelee na jitihada hizo.
|
|
Records 1 to 1 of 29 |
|
|
|
|
|